Friday, February 25, 2011

Facebook, simu za mkononi zinavyoumiza watu katika mapenzi.

TUPO kwenye muktadha wetu unaosema: “Facebook, simu za mkononi zinavyoumiza watu kwenye mapenzi.”
Somo hili ni zuri, ndiyo maana baada ya kutoa sehemu ya kwanza, kwenye toleo la Jumatatu wiki hii, nilipata simu na meseji nyingi kupindukia.

Nasema ahsante kwa pongezi na naomba uambatane na mimi, ili tuendelee kutoka pale tulipoishia. Wiki iliyopita, nilitoa mifano kadhaa iliyopo nyuma ya migogoro ya simu za mkononi.

Hata hivyo, nimeona mada hii niichambue katika maeneo mawili. Wiki hii niendelee na somo la simu, halafu likiisha nitaanza na Facebook.

Niliandika jinsi watu wanavyotengana au wanandoa kukosa suluhu kwa sababu ya simu. Namna baadhi yetu tunavyokosa uhuru na amani na kuishia kuwapiga marufuku wenzi wetu wasishike ‘viselula’ vyetu, tukihofia siri zetu kugundulika.

Na tatu ‘niliwabonda’ wale wataalamu wa ‘kusevu’ namba za wenzi wao wa pembeni kwa majina tofauti, wanaume kuandika ya kiume na wanawake kuweka ya kike. Haya ni mapenzi ya mashaka.

‘Ki ukweli’ simu za mkononi ni utandawazi uliojaa chembechembe nyingi za sumu katika uhusiano wa kimapenzi na hii imetokana na watu wengi, kukosa ustaarabu na kuzitumia kuwasaliti wenzao
Hata hivyo, dhamira ya mada hii ni kukuandikia mbinu kadhaa zitakazokufanya wewe uishi na amani, bila kuzichukia simu kama dada yangu, Jasmin Mdanzi wa Nyakato, Mwanza ambaye sms yake niliiandika wiki iliyopita.

Pamoja na mbinu hizo, ningependa nikufahamishe kuwa haya nitakayoyaandika kama wewe utashindwa kuyafanyia kazi inavyotakiwa, hakuna kinachoweza kufanyika.

Mosi, wewe na mpenzi wako mnapaswa kuwa na uelewa mkubwa, kwa kutambua ukweli. Pili ni kuacha papara, mambo ya kusikia simu ya mpenzi wako inaita, unairukia na kutaka kujua anayepiga au aliyetuma ujumbe, vimepitwa na wakati.

ANGALIZO; Inawezekana akawa hana tabia ya kucheza mechi za nje, lakini wivu wako wa kupitiliza ndiyo unaomfanya ashindwe kuwa huru. Hata Zainab ambaye ni dada yake ofisini, anamuandika Zidane kwa sababu ukikuta jina la kike hauwezi kumuelewa hata akuambiaje.

Hujawahi kuona, mtu anamuelewesha kuwa fulani ni dada yake ambaye hushirikiana kwa ukaribu ofisini, lakini mama nyumbani haelewi, hapo matokeo yake ni jamaa ‘kumsevu’ Ramla kama Ronaldo.

Pointi ni hizi zifuatazo, naamini ukizisoma kwa herufi katika kila mstari, utapata kile kitu ambacho binafsi nimekikusudia, pia utaweza kuondoa migogoro isiyo na ulazima.

KUJIAMINI!
Inawezekana wewe ni muaminifu katika mapenzi yako, lakini tabia yako ya kujishtukia mara kwa mara kila anapokuomba simu, inamfanya aanze kuwa na mashaka juu yako.

Anajiuliza, kwanini haupendi ashike simu yako? Elewa kuwa jibu atakalolipata hapo ni kuwa kuna mchezo mchafu unaomchezea, na unaufanya kupitia simu ndiyo maana unailinda kama nguo ya ndani ambayo huivua wakati wa kuoga tu.
Wasilia na nico trac kama una mada ya kupost na nzuri 0716276000 or 0755451999

No comments: