Sunday, December 30, 2012

Unavutia lakini hupati mpenzi wa kweli, tatizo ni nini?

NIANZE kwa kuwakumbusha kwamba bado kidogo sana kile kilio chenu kifikie tamati, ni juu ya ujio wa kitabu changu kipya kilichokusanya mada nyingi pamoja na Love Messages zenye tiba ya penzi linaloanza kupoteza mwelekeo.

Kinahusu msichana mmoja mrembo (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka 29, lakini aliyeteswa na mapenzi sana. Watu mbalimbali walitoa ushauri na maoni yao, wengine wakaomba wawe wachumba. Mh! Haya bwana, ninachokifanya ni kuchapa baadhi ya sms kisha mwenyewe ataamua la kufanya. Hebu tuone sms za wasomaji kumi tu...

Msomaji wa kwanza: Bibie hii ndiyo hali ya dunia, kumbuka kuna msemo unasema, hakuna kizuri kinachokosa kasoro. Steven Mhehe, Zanzibar.

Msomaji wa pili: Huyo binti kuna mahala anakosea, uzuri alionao kama wanavyosema hautoshi, inawezekana si mnyenyekevu katika uhusiano, anakosa lugha ya mapenzi n.k. Ajaribu kuangalia maeneo hayo. Bunge Nyamonge, Ukonga Dar.

Msomaji wa tatu: Anko Jose, mimi naitwa Deo wa Dar, naomba namba ya huyo dada wa Tanga, nataka kuzungumza naye.
Msomaji wa nne: Niilichojifunza hapo ni kwamba watu wapeane mapenzi baada ya ndoa na siyo kabla. Omary Juma, Igogo, Mwanza.

Msomaji wa tano: Nimejifunza kwamba, si mwanaume utakayemuona anaweza kuwa na mapenzi ya kweli, pia tusipende kujirahisha kwa wanaume, kwa sababu mwanaume akishakufunua na kujua ulivyo, imepita. Nawashauri wasichana wenzangu tuwe na msimamo. (Hajataja jina lake).

Msomaji wa sita: Huyo dada wa Tanga anaonekana kuwa na matatizo kama yangu, mimi ni mwanaume msomi wa Chuo Kikuu, nina miaka 39. Nimeachana na mke wangu wa ndoa kwa matatizo. Niunganishe na huyo dada tunaweza kufarijiana! Mpe namba yangu, nitamweleza nilipo.
Msomaji wa saba: Pole sana dada zetu mlio wazuri kupindukia, kwani wanaume wengi huwa waoga kuwa katika uhusiano na watu wazuri, wakihofu kuachwa. Ninachoweza kusema ni kwamba sisi wanaume ndiyo wabaya wa kuwachezea watoto wa watu na mwisho wanaonekana kama malaya tu!

Msomaji wa nane: Naitwa Ngosha kikazi nipo Arusha, lakini wikiendi hii nipo hapa Dar. Mimi ni Mkristo, miaka 27, nimezaliwa Bugando. Naomba namba ya huyo dada, kama yupo tayari kufunga ndoa.

Msomaji wa tisa: Wanawake wengi hutumia uzuri wao kwa kufikiri kuwa kila mwanaume anayemtaka kimapenzi humpenda kwa ajili ya uzuri alionao, matokeo yake humtumia kimapenzi na kumuacha. Anachotakiwa kufanya huyo dada ni kwamba, hakuna mwanamke mwenye matatizo katika suala zima la mapenzi, kwani hayo mambo ni ya kujifunza hata kama hujui. Afahamu kwamba wanaume wote aliowahi kukutana nao, hawakumpenda bali walimtamani, awe makini sana wakati wa kuanzisha uhusiano mpya na mwanaume mwingine na asitumie uzuri wake kuwa kigezo cha kupendwa na kila mwanaume.

Zuhura M., Dar es Salaam.
Msomaji wa kumi: Tunajifunza kwamba, uzuri si kigezo cha tabia, maana unaweza kuwa mzuri lakini ukawa mbovu wa tabia. Timilai Shemalamba, Tanga.

KUTOKA KWA SHALUWA
Ushauri wa wote niliochapa meseji zao, nimeuacha kama ulivyo na msomaji wangu huyo ana uamuzi wa kuamua nini cha kufanya.

Aidha, kuna ambao mmeomba namba zake, kwakuwa sina mamlaka ya kutoa namba za mtu, nimechapa namba za waombaji ili kama dada huyo akiridhia mwenyewe atakutafuta. Haya twende moja kwa moja kwenye funzo linaloonekana hapo.

Tunaona moja kwa moja makosa ya kuruhusu mwanaume aujue mwili wa mpenzi wake mapema. Suala la uaminifu huanzia mbali rafiki zangu, ukionekana huna msimamo, rahisi kudanganyika, tafsiri yake inakuwa kwamba unaweza kuwa hivyo kwa wanaume wengi zaidi.

Nani anapenda kuwa na mwanamke wa kuchangia? Nani anapenda kuwa na mwanamke anayedanganyika kirahisi? Utadanganyika na wangapi? Wanaume wanapenda kuona unakuwa mgumu kuruhusu mwili wako kuchezewa! Ndiyo wengi wanajisifu wakiwa kwenye ndoa zao.

Ndiyo maana utasikia mwanaume akijisifu kwa mkewe: “Mke wangu ulikuwa mgumu sana, lakini nilitumia kila njia kukupata...” au “Ah! Ulinisumbua sana mke wangu, lakini nashukuru nimekupata.” Kwanini yote haya? Kwa sababu anahisi yupo na mwanamke thabiti, mwenye msimamo na asiyeyumbishwa.

Sina shaka umepata kitu kipya kichwani mwako. Naomba niwaache, hadi wiki ijayo tena nitakapokuja na mada nyingine.

Wednesday, July 25, 2012

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII



 

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku.
Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

 
MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha  siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
 
Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya  maisha ya  ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia  ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.
 
WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini  wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa  anatabia mbaya. Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya  wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume  ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
 
WENYE UCHU NA MAENDELEO
 
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini. Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
 
WASIOPENDA MAKUU
 
Kuna  wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"  Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama  ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho  nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

 
Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa  kuwaoa.  Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa  tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi  ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.
Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
 
WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
 
Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
 
Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
 Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam. Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.
Via http://irenemwamfupejamii.blogspot.com/p/mahusiano.html

WANAWAKE HUPENDA KUFANYA MAPENZI JUMAMOSI SAA 5 USIKU



Utafiti mpya na wa kina kabnisa umeonesha kuwa asilimia 85 ya wanawake duniani kote huwa wanafanya mapenzi saa 5 usiku kila Jumamosi.

 Kwa mujibu wa utafiti huo uliozingatoa vigezo vya kibinadamu, saa 5 usiku siku ya Jumamosi ndiyo muda ambao wanawake wengi wanajisikia hamu ya kufanya tendo la ndoa kuliko muda mwingine wowote katika siku saba za wiki.
Asilimia 85 ya wanawake waliohojiwa katika utafiti wa kiafya, walikiri kufanya kujisikia zaidi hali ya kutaka kufanya mapenzi muda huo katika siku ya Jumamosi kuliko muda mwingine wowote.

Utafiti mkubwa ulifanywa katika nchi za Kusini Mashariki, Magharibi Mashariki  na meneo ya Scotland ambapo wanawake walisema muda huo mwili wenyewe huwa unahitaji kukutana kimwili na wanaume wenye uzoefu wanalijua hilo bila kuombwa wanapokuwa kitandani.


Aidha, utafiti mwingine umebaini kwamba, asilimia 75 ya wanawake duniani kote wanapenda kufanya mapenzi mara tatu kwa wiki, ikiwemo siku hiyo ya Jumamosi.
Kazi iko pale ambapo utafiti umeonyesha kuwa asilimia 25 ya wanawake dunaini kote hupenda kufanya mapenzi kila siku katika muda wa siku saba. Kundi hili la wanawake ndilo linalohusika zaidi na usaliti katika uhusiano na pia watafiti wanadai kuwa, katika asilimia hiyo 25, 23 hukumbwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.

Tuesday, June 19, 2012

7 Ways to Build Trust in a Relationship



Are you involved in a relationship where you completely trust your partner? If you answered “no,” then this is the article for you. Relationships require you to have a great deal of trust for your partner, and they should have the same trust toward you. Many people think that in order for a relationship to thrive there needs to be continual variety and less routine. This is not necessarily the best way of thinking. In fact, the most stable and successful of relationships rely on routine. Predictability in a relationship is much more important than variety. It allows for the development of trust. Are you at a point in your relationship where you are ready to allow yourself to trust your partner? If so, then here are 7 concrete ways for you to improve the level of trust in your relationship.


The first way that you can build trust in your relationship is to allow yourself to look at predictability as a positive thing. This goes against the notion that the most successful relationships are those between partners that “spice things up” all the time. Think about it. If you are accustomed to your partner always sending you a goodnight text and all of a sudden they stop doing that, what are you going to think? Perhaps they stopped so that you will appreciate the goodnight more, or maybe they have started to spend time with someone else. The human mind has a unique way of interpreting changes within the relationship. This can lead to a steady unraveling of trust between people. Remember, being predictable does not mean that you can’t try a new restaurant, or surprise your partner with a weekend trip, or a gift. Being predictable simply means that the way you and your partner interact with each other needs to remain consistent in order for trust to be built.
The second way that you can build and strengthen the trust in your relationship is to make sure that your words always match your actions. If you tell your partner that you are fine when clearly there is something wrong your partner is not going to hear your words. They are going to see the frown on your face and sense the tension in your voice. Next, you need to make sure that your words always match the message. This means that your partner needs to hear the words which match your body language. If you say you are happy but you are frowning, your partner doesn’t hear your words, he or she sees your face and the tone in your voice. When actions and words match the ability for trust to grow is very strong.


The third thing that needs to happen in order for trust to grow is for you to have a belief in the competency of your partner. If this is not present, you will never be able to have the trust that you need for the relationship to thrive. You and your partner will always need to be truthful with one another. It may seem scary because sometimes the truth can hurt. However, when it is lovingly communicated, the truth is never destructive. Everyone has different strengths and weaknesses. Knowing what your partners’ strengths are and believing in the competency of your partner will ensure that you never violate the trust within your relationship.


The fourth way that you can build trust is by not keeping secrets. Secrets are known to destroy the trust in a relationship. Both you and your partner need to be open and honest with one another. It takes much more emotional energy to keep a secret then it will if you tell your partner. This energy would be better spent if it was used toward building the relationship. In addition, sharing your secrets with your partner enables the two of you to have a better understanding of each other, thus increasing the level of trust between the two of you.


The fifth way that you can increase the trust in your relationship is by communicating to your partner what your needs are. Don’t make them guess what you need, because this will usually lead to disappointment for you when your partner doesn’t give you what you need, as well as frustration for them when they can’t figure out what you need. It is much easier if the two of you can simply let each other know your needs. If you hide your needs, you will never be happy within your relationship. Remember, allowing your needs to be known does not make you selfish. Instead it allows for a new level of trust and open communication between you and your partner.
The sixth way that you can increase the trust in your relationship is by learning to say no. It is a wonderful thing when your partner is able to voice their needs. However, this does not mean that you need to say yes to each and everything that they need. How will your partner learn to respect you if you say yes to everything? You need to remain true to yourself and not become completely subjugated to your partner. Listen openly to their needs, and expect them to do the same for you. Don’t become a doormat, or expect your partner to become one. An equal relationship is another way of building the trust within a relationship.


The final way that you can build trust in your relationship is by always pursuing growth. Think about it. When you plant a flower there are steps that you take. You begin by digging in the dirt and making sure that the roots have a strong and healthy foundation. In a relationship, “digging in the dirt” can sometimes be a painful experience. However, through that pain we are preparing a strong and healthy foundation for our relationship. Don’t fear turmoil, or sadness, or questions that will arise within your relationship as these are the “fertilizer” for relationship growth. Always embrace that which is difficult, because nothing that is worth it will ever come about easily.
When you and your partner make the commitment to work on the trust within your relationship, you are bound to encounter some pain and heartache. You may hear things that you don’t want to hear, however as you work through this pain as a couple you will not only become stronger as an individual, and you will become stronger as a couple.


Wednesday, June 6, 2012

Mwanamke anayefaa kuolewa ni yupi hasa?

Add caption

NI siku nyingine tena tunakutana katika ukurasa huu kwa lengo la kupeana mawili matatu juu ya mambo ya uhusiano na mapenzi. Nawashukuru wote ambao mmekuwa mkinipa changamoto mbalimbali juu ya uboreshaji wa safu hii.

Rafiki zangu, leo nataka kuzungumzia jambo muhimu sana katika maisha ya mapenzi hasa kwa vijana ambao wanafikiria kuoa. Natambua kwamba wengi huwa wanafikiria sana kuhusu aina ya wanawake wanaofaa kuolewa.

Katika fikra hizo, kuna ambao hufikiria zaidi suala la mazingira mwanamke husika alipozaliwa na kukulia. Yaani wanafikiria kuhusu ubora wa mwanamke aliyezaliwa kijijini au mjini.

Kila mmoja huwa ana wazo lake, akiwa na utetezi wa anachokiamini, lakini ukweli halisi ni yupi? Wewe unaonaje?
“Mimi nimeoa kijijini kwetu huko Saweni Juu, Same naishi na mke wangu mwaka wa tatu huu kwa amani tele. Ananiheshimu, ni mchapakazi na sijawahi kusikia tetesi mbaya kuhusu yeye hata mara moja. Nampenda sana kwa kweli,” Oscar Genesis, mkazi wa Tandale Kwa-Mtogole, Dar alisema alipokuwa katika mahojiano nami.

Wakati Oscar akisema hayo, Francis alikuwa na haya ya kusema: “Kuoa mwanamke kijijini ni hatari sana, unaweza kumleta mjini akiwa hajui kitu, lakini akishaujua mji tu anaanza kukusumbua. Mimi naona ni bora mwanaume akaamua kuoa mwanamke wa mjini ambaye anajua kila kitu, hatamsumbua maana kila kitu anakuwa ameshamaliza.”

Rafiki zangu, ukweli ni upi hapa? Kwanza nitaanza kwa kuwachambua wanawake hawa waliokulia katika mazingira mawili tofauti kabla ya kuendelea na uchambuzi zaidi.

UKWELI KUHUSU MWANAMKE WA KIJIJINI
Hivi ni kweli kwamba mwanamke wa kijijini ni bora zaidi kuliko wa mjini? Wapo wanaofikiria hivyo, lakini hapa nitakupa mazuri na mabaya yake, ambayo bila shaka yatakupa mwanga wa uchaguzi wa mke bora.

Mwanamke huyu anaelezwa kuwa na heshima kupindukia, siyo mkaidi, muelewa na mwenye nidhamu sana kwa mumewe. Hana makuu, hapendi starehe, anajali familia, ndugu wa mumewe na hata marafiki wa karibu na mume wake.
Anajua shughuli za nyumbani kama mke, lakini pia ni mtafutaji mzuri kwani mara zote hujishughulisha na biashara ndogo ndogo au kilimo.

Ni mwepesi kuelewa mambo, hasa kama anakatazwa au kuonywa. Anajua nafasi yake kama mke na ‘anacheza’ ipasavyo katika nafasi hiyo. Anaweza kuishi maisha ya aina yoyote.
Wakati uzuri huo ukianishwa, pia yapo mabaya ambayo yanasemekana mwanamke wa aina hiyo anakuwa nayo. Inaelezwa kwamba, asilimia kubwa ya mwanawake wa kijijini hajaenda shule!
Wengi huishia darasa la saba na kuolewa au kubaki nyumbani. Hili huvumbua kasoro nyingi nyuma yao, lakini kubwa zaidi wanakuwa hawana ufahamu wa mambo mengi.

Hawajui dunia inaendaje, mawazo yao siyo endelevu na siyo mapana. Hawana mipango ya muda mrefu, wanawategemea zaidi waume zao kwa kila kitu.
Baadhi yao huamini kuolewa ndiyo kila kitu na mume ndiyo kila kitu katika nyumba. Kwamba anaweza kufanyiwa kila kitu na mumewe kwa sababu eti ni mume! Siyo mwepesi wa kugundua makosa au matatizo.

Ni rahisi kufanya jambo baya na kung’amua baadaye sana ubaya wa jambo alilolifanya. Siyo mjanja, ni mzito kifikra. Muoga kujifunza. Baadhi yao hupelekwa unyagoni ambapo hufundwa na kuelekezwa anayotakiwa kuyafanya kama mwanamke. Mara nyingi hupelekwa huko akiwa na umri wa kuanzia miaka 13-15, akitoka huko anaamini tayari yeye ni mtu mzima!

Anaanza kufanyia mazoezi aliyofundishwa. Mafunzo yanayotolewa huko yanadaiwa kuwa si mazuri sana, kwani mtoto hufundwa mambo mazito ambayo anapaswa kufundwa mwanamke ambaye anajiandaa kuingia kwenye ndoa. Kuharibikiwa huku mapema, wakati mwingine kunaweza kumuathiri hata anapokuwa mtu mzima na familia yake.

Haya ndiyo baadhi ya mambo yanayodaiwa kuwa mabaya na mazuri ya mwanamke wa kijijini. Kwa leo tuishie hapa, wiki ijayo tutaendelea katika sehemu ya pili ya mada hii.

Ni ngumu kupata raha ukiingia kwenye ndoa kwa unafiki


"NI lazima niolewe kwa sababu wadogo zangu wameshaolewa, aaah hapana bwana wadogo zangu wameshaoa kwa hiyo ni lazima na mimi nitafute mtu wa kuoana naye,”ndivyo wanavyojisemea baadhi ya watu.
Kuna wengine wanaoa kwa sababu wameshinikizwa. Lakini ukweli ni kwamba ndoa yoyote ambayo haina upendo wa dhati, ni kosa kubwa.
Katika hali kama hii baadhi ya watu huwa tayari kuoana na yeyote anayepita mbele yake hata bila kuangalia kwa makini kama kweli mtu huyu ni mzuri kwake au la.
Hali hii ya kukubali kuolewa kwa sababu wadogo zako wameolewa, huchangia kasi ya ndoa kuvunjika, kwa sababu watu wanaoana pasipo kupendana kwa dhati.
Ndoa ni nzuri, lakini lazima uelewe kuwa unapaswa kuoana na mtu kwa sababu umemuona anakufaa hasa baada ya kumchunguza kwa makini na kuamini kweli anakufaa.
Usiingie katika mapenzi kwa unafiki, unafiki wa kusema aaah kwa vile baba amesema nikikataa ataniona sina adabu....kumbuka ndoa ni maisha yako si ya baba yako wala mama yako. Ukipata shida utakayeumia kimaisha ni wewe, si mwingine.
Uongo pia ni suala baya katika uhusiano…mwingine ni mnywaji mzuri wa bia na aina nyingine ya vileo lakini ukimuuliza anakwambia mimi simwi wala sivuti, naye anakwambia aaah hata mimi bwana, yaani sipendi kabisa kunywa.
Kama wewe ni mnywaji, sema mimi nakunywa ili mwenzi wako ajue aina ya mke au mume ambaye atakuwa naye. Ingawa ni hatari zaidi kwa mwanamke kulewa, kuliko mwanaume hasa katika suala la uaminifu wa ndoa, lakini maisha ni makubaliano.
Ni rahisi mwanaume mlevi kubaki mwaminifu, lakini ni vigumu kwa mwanamke mzuri mlevi kubaki mwaminifu kwa ndoa yake, kama unabisha shauri yako.
Ninachotaka kusisitiza hapa ni umuhimu wa mtu kuwa muwazi hasa pale wanapoanzisha urafiki, hii itakusaidia hata katika siku za baadaye za uhusiano wenu kuishi kwa amani.
Eeeh bwana maana mumeo atakuwa anajua kwamba nimeoa mke mlevi, nimekubali, hakutakuwa na ugomvi, maana ulishamwambia kwamba mimi bila kunywa usingizi haupandi...siku ukifungwa jela au ukiumwa sijui utalalaje ? Mimi sijui, lakini ninachotaka kusema kwenye kipengele hiki ni kwamba wapo watu wanasema hivyo kwamba eti asipokunywa hajisikii vizuri, kitu ambacho si kweli.
Unafiki mwingine ni wa tabia katika mazungumzo nk, ndugu yangu kama unaelekea kuoa au kuolewa, ni vizuri siku moja tafuta uwezekano wa kugombana na mwenzi wako, uone kauli zake zikoje, anajibu vipi malalamiko.
Kuna wengine wanajifanya wakimya, lakini wana lugha chafu kana kwamba wametoka kwenye shimo la choo. Ni wiki mbili tu zilizopita kuna mama mmoja alimchukua binti kanisani awe mfanyakazi wake wa ndani.
Huyo binti alikwenda kanisani, kweli walikuwa wakimsifia kuwa ni mzuri kwa namna alivyokuwa akionekana....siku moja kwa bahati mbaya bosi wake alipata safari ghafla kiasi kwamba aliacha fedha kidogo nyumbani.
Akiwa huko mbali na nyumbani akapata ujumbe mfupi kutoka kwa mfanyakazi huyo wa ndani ??ndio fedha gani hiyo umeniachia, mimi huwa sinywi maji ya bomba, nitumie fedha ya kutosha ninunue maji ya dukani, nikinwa ya bomba tumbo linauma?
Huo ni ujumbe wa kutoka kwa binti ambaye kanisani anaonekana ni mtakatifu. Kama hiyo haitoshi wakati bosi wake yuko mbali ikabainika akawa analala na kijana mmoja wa mtaani hapo, bosi akalazimika kumfukuza kwa sababu ya kuona anakwenda kinyume na alivyokuwa akimtarajia.
Unafiki hauko tu katika mapenzi, bali hata maofisini, mwingine anaweza kukuchekea na ukaamini ni rafiki, kumbe anakuchimba...eeeh bwana wengine ni maarufu wa kutangaza mabaya ya wenzao, huku wao wakijiona ni watu safi, wajuaji wa mambo nk.
Katika maisha ni vizuri kuwa kama ulivyo, simamia kwenye ukweli wala usikubali kuingia kwenye uongo ili upate hiki na kile, maisha tunayoishi ni mafupi, uko leo, hujui kama kesho utafika, yanini kuwa mnafiki? Yanini kusengenya wengine? Yanini kuwa mtu wa majungu, badala ya kuangalia mambo yako ambayo yatakusaidia uwe na maisha bora zaidi kuliko ulivyo sasa?
Tangu mwaka uanze umeshateta watu wangapi? Umeshafanya unafiki mara ngapi? Je, kati ya maneno unayozungumza kwa siku, mengi ni ya aina gani....unafiki, uongo au heri kwa wengine? Mimi sijui, lakini wewe unalo jibu, lakini kwa vyovyote itakavyokuwa ni vizuri katika maisha pendelea kuachana na tabia za kinafiki.

Monday, June 4, 2012

Hata kama yuko mbali, muamini, usimsaliti mtadumu!


Nina uhakika baadhi yetu tuna wapenzi ambao wako mbali, hilo lisikupe shaka. Bado unaweza kuendelea kuliboresha penzi lako na mwisho kutimiza ndoto zenu mlizojiwekea za aidha kuoana kwa wale ambao bado wapo wapo au kudumisha ndoa yenu kwa ninyi mliooana.

Katika hili kuna mambo mawili ya msingi ambayo leo nataka
kuyazungumzia ili kuhakikisha uhusiano wenu hautetereki.  
Kwanza, hakikisha humsaliti mpenzi wako. Ukitaka kufurahia mapenzi, lazima usiwe msaliti. Upo msemo usemao, ukimsaliti mpenzi wako ujue nawe utasalitiwa, sasa ili uepukane na hilo ni vyema ukajiwekea dhana ya uaminifu wewe kama wewe kwanza.

Jisemee mwenyewe; “Kwa nini nimsaliti mpenzi wangu? Nampenda sana na najua nikimsaliti hatajua, lakini na yeye akinisaliti je?” Tafakari maneno hayo kwa makini sana, naamini kuna kitu utajifunza.
Jichunge mwenyewe, usikubali kabisa kuharibu thamani yako kwa kumruhusu mtu mwingine aujue mwili wako kwa kuwa tu umesikia ‘hamu’.

Kumbuka mwili wako ni kwa ajili ya mpenzi wako pekee, endelea na dhana hiyo siku zote utakazokuwa mbali naye, naamini utafurahi!
Kwa kufanya hivyo, hutaona faida yake kwa haraka lakini fikiria hili kwa makini, kama wewe umeamua kuwa mwaminifu kwa mwenzi wako kwa kutambua thamani yake, kwa nini Mungu asikulindie huko alipo? Ila lazima ufahamu jambo moja, Mungu anaweza kukulindia mwenzi wako ikiwa naye anakupenda kwa dhati na ana nia ya kuishi na wewe hapo baadaye.

Jambo lingine la msingi ni kujenga uaminifu kwake. Baada ya kuhakikisha kwamba humsaliti, sasa ni wakati wako wa kuhakikisha unamwamini katika kiwango cha mwisho. Usimwoneshe mashaka sana na nyendo zake. Wakati mwingine unaweza kumpigia simu asipokee, hilo lisikuchanganye.

Kuna baadhi ya watu, akimpigia simu mpenzi wake akiona hajapokea, tayari hisia zake zinakuwa mbali na muda huo huo anamwandikia meseji mbaya za ukali na kumtuhumu kwamba anajua huko aliko anamsaliti! Huna haja ya kufanya hivyo, onyesha kumwamini.

Kama umempigia na simu yake haipatikani, ni wakati wako wa kumwandikia meseji ya kumpa pole kwa kazi kutokana na kutambua kwako kwamba muda huo alikuwa bize.

Mwandikie hivi; “Natambua ni majukumu mengi uliyonayo muda huu ndiyo yaliyosababisha ushindwe kupokea simu yangu, usijali kwa hilo. Nakupenda sana na natambua kwamba mimi ndiye mwenye jukumu la kuhakikisha nakuwa karibu na wewe kwa kila kitu, nakupenda mpenzi wangu, kazi njema.”

Ujumbe huo utamfurahisha, kama alikuwa na nia ya kukusaliti, hawezi kufanya hivyo kwani atakuwa anajua anamsaliti mwenzi ambaye anamwamini katika kiwango cha mwisho.

Kumuamini kwako kutamfanya aone ni jinsi gani ambavyo wewe mwenyewe unavyojiamini na usivyo na wazo la kumsaliti! Kwa nini yeye akufanyie hivyo? Lazima atabadilisha wazo lake.

Mpenzi msomaji wangu, hayo ni mambo mawili ya msingi ambayo unatakiwa kuyazingatia pale unapokuwa mbali na mpenzi wako. Kumbuka kuwa mbali na huyo uliyetokea kumpenda haiwezi kuwa sababu ya nyie kutengana.

Mtatengana tu endapo hakuna mapenzi ya dhati kati yenu lakini kama mmependana kiukweli kutoka mioyoni mwenu, hata muwe mbali kwa muda mrefu kiasi gani, bado hakuna cha kuliua penzi lenu.

Utamjuaje mwenye mapenzi ya kweli?


Nimeandika mada hii kutokana na watu wengi kushindwa kutofautisha kupendwa kweli na kutamaniwa. Wapo walioingia mkenge kwa neno hilo hasa walio wageni katika uwanja huu wa mahaba. Ukiambiwa unapendwa basi unachanganyikiwa na kusahau maneno matupu hayajengi nyumba.

Nina maana gani?

Watu wengi wamekuwa wakitumia neno hili kama mtego wa kumpata mtu, kwa kujifanya anakupenda sana na nahau nyingi za mapenzi ambazo zinaweza kukufanya masikio yako yazibe na kuona nani kama wewe.

Siku zote mtafutaji ana lugha tamu ya mapenzi na kabla ya kutamka lolote lazima atangulize nakupenda sana na kuongezea ajuavyo. Hii si mara moja watu kuingia mkenge inapotokea wanakutana na hali hiyo.

Lazima uelewe serikali ya mwili wako inakutegemea wewe, ukiipeleka vibaya lawama zitakuwa juu yako. Usiwe na papara ya kutoa uamuzi wa kukubali uambiwavyo unapendwa bila kufikiria kwa kina. Hakuna hata siku moja mtu anayekutaka kimapenzi akuambie anakuchukia.

Fikiri kabla ya kutenda na kuona kauli uliyopewa ina nia gani na wewe, kweli anakupenda au anataka kukuchezea na kukuacha.

Katika uchunguzi wangu nimegundua wengi hupima kwa masikio juu ya kile aambiwacho na si kufikiria nini hasa kilichomvutia aliyekutamkia maneno hayo. Japo kakutamkia anakupenda, ni vema ukafanya kadiri uwezavyo kupata muda kufikiria kwa kina kabla ya kutoa uamuzi wowote ambao unaweza kukufanya uwe na faida au hasara.

Neno nakupenda siyo mapenzi kamili, bali tabia ya mtu na kuonyesha kweli anakupenda kwa dhati. Akupendaye huwa hana haraka ya kufanya ngono, hufuata taratibu zote ili mradi kujenga uaminifu moyoni mwako.

Hii hutokana na kuwa na uhakika wewe ni wake, hana hofu ya kutanguliza ngono mbele katika uhusiano wenu wa kimapenzi. Ukiona umekutana na mtu anayetanguliza ngono baada ya neno nakupenda huyo hakupendi bali anakutamani.

Tumekuwa tunatumia neno nakupenda kama kiwakilishi cha ujumbe wa mapenzi na si penzi kamili.
Mapenzi ya kweli ni ya vitendo na si maneno, anayekupenda utamjua tu wala hajifichi. Atakuwa mpole, mwenye huruma, anayekujali, muaminifu na mtu aliye muwazi mwenye kukupa uhuru wa kumjua kwa undani ili kukuondoa wasiwasi.

Mapenzi mengi ya siku hizi yamekuwa ya usiri mkubwa yenye mipaka. Kama kweli anakupenda kwa nini akudanganye na akuwekee mipaka ya kumjua? Wakati huo mdomoni kwake ana kila nahau tamu za kimapenzi na kulitamka neno nakupenda kama kiwakilishi.

Huyo si mkweli wala hana mapenzi bali ni muongo aliyejificha nyuma ya neno nakupenda. Kuwa macho na watu hawa sipendi kesho uniulize swali hili.source ya mada hii,Muandishi Joseph shaluwa

Thursday, May 31, 2012

Je, wivu katika mapenzi unaleta maana?

By Miki Da BataBoyz PrezDent



Kama mmeweza kujitoa mhanga kwa kiasi hiki sababu ya penzi, kwanini msioneane wivu?
Assalam Alaikum! Ni furaha yangu kwa mara nyingine tena kukutana nanyi wapendwa wasomaji wa safu yetu hii ya uwanja wa mapenzi. Tumshukuru Muumba wetu kwa kutujaalia uhai na afya njema, lakini zaidi ya hapo tumshukuru pia kwa kutuumbia kitu mapenzi au sio?
Siku zote hatutaacha kuzungumza juu ya mapenzi kwani ni ukweli usiopingika kwamba mapenzi ndio maisha yetu. Tunafanya kazi usiku na mchana, tunahangaika huku na huko, lakini mwisho wa siku tunafikiria jinsi gani tutapata kuboresha na kufurahia maisha na wapenzi wetu. Tunafikiria pia ni jinsi gani tunaweza tukapata utulivu na amani katika maisha ya kimapenzi na wapenzi wetu, waume zetu au wake zetu katika siku zote za maisha yetu.
Wiki hii nimeona ni vyema tukabadilishana uzoefu juu ya suala zima la wivu katika mapenzi. Mtakubaliana nami kuwa suala la kuwa na wivu kwa mpenzi wako ni jambo lisilokwepeka hasa kwa sababu kubwa ya kuaminika kwake kwamba kuwa na wivu ni moja ya kigezo cha kuonesha ni jinsi gani unampenda mpenzio na kwamba hauko tayari kwa namna yoyote ile kushea na mwingine ndio maana wanawake wengi hawataki kusikia suala la ukewenza kabisaa! Hata kama jambo hilo limepewa baraka zote na dini au tamaduni zao.
Lakini kubwa katika wivu ni ile kutokuwa tayari kuona tunasalitiwa na wapenzi na hasa kwa wale tunaowapenda ukweli toka moyoni mwetu na zaidi ukute ndo tumeshawagharamikia kiasi cha kutosha na kujitoa kwao kwa kila kitu!
Umeshawahi kusikia kauli kama “Jamani mke (au mume) anauma! Au kauli kama mke wa mtu sumu” na hugeuka sumu kweli hasa pale “unapobambwa” na mali za wenyewe, kufanyiwa “kitu mbaya” inakuwa sio jambo la ajabu sana.
Niwaambie kitu wapenzi wasomaji! Mapenzi bwana ni “full uchoyo, ni full kujipendelea! Mpenzi wanaume kwa mfano, anaweza kufikiria kwamba ni yeye tu ndiye anayestahili na anayeweza kumfanya mpenzi wake acheke na kufurahi.
Na kwamba akitokea mwanaume mwingine akapata nafasi ya kumfurahisha mpenzi huyo hata katika stori za kawaida tu, unaweza ukasikia akisema, “Hivi wewe mna nini na huyo jamaa, mbona unamchekea chekea hivyo, au…!” Hiyo ndiyo choyo ya penzi, na kikubwa kinachofanyika hapo ni ile tu kujaribu kulinda maslahi binafsi.
Pamoja na ukweli kwamba tabia ya wivu inapozidi hugeuka kuwa kero, lakini kabla hatujafika huko hebu tuangalie nafasi ya wivu katika mapenzi yetu. Yaani swali ni kwamba, je! Wivu katika mapenzi unaleta maana?
Nionavyo mimi wivu ukitumika vizuri unaleta maana na una nafasi muhimu sana katika mapenzi kwa sababu zifuatazo:
Huonesha kujali
Sote tunaamini pasipo na wivu hata chembe, hapana mapenzi ya kweli. Kumuonesha wivu mpenzi wako ni kumjulisha ni kiasi gani unamjali na kumpenda na kwamba yeye ni mtu maalum sana kwako.
Jamani, mahali penye mapenzi yasiyo na wivu hata kidogo, panatia shaka! Na mara nyingi majibu yake ni kutokuwa “sirias” katika uhusiano huo au huenda kuna kupitisha muda tu na kwamba labda hakuna “future” na mpenzi huyo au ni dalili ya kuchuja kwa penzi.
Kuthamini uhusiano
“Sio kama sikuamini dear, bali wivu wangu kwako ni katika kuuthamini uhusiano wetu, mimi na wewe ni umoja wenye thamani kubwa, tusiruhusu kuuchezea nje yetu! Huu ni mfano wa ujumbe unaoonesha maana na nafasi ya wivu katika mahusiano ya kimapenzi.
Kukumbushana
Kauli au matendo yanayoashiria kumuonesha wivu mpenzio yanasaidia kwa kiasi kikubwa kumfanya mwenzi wako “asijisahau” katika jukumu la kulienzi penzi lenu hata akiwa mbali ya upeo wa macho yako.
Kujijengea heshima
Kwa namna moja au nyingine, wivu pia huweza kukujengea heshima. Kwa mfano mume mwenye wivu na mkewe hujijengea heshima ya kwamba kweli anamjali na kumpenda mkewe lakini pia anaweka mazingira ya kutosumbuliwa kwa mke wake huyo kumjengea heshima yake kama mke wa mtu.
Husaidia kubadilisha tabia
Ukiwa na wivu, unaotokana na mavazi “tatanishi” anayopendelea kuvaa mpenzi wako kwa mfano, huenda ikasaidia kubadili tabia yake.
“Ni kweli umependeza na umetoka “chicha” ile mbaya mpenzi, lakini mh! Naogopa wanaume wakware watakusumbua honey, unaonaje ukavaa simpo tu?” Kama anakupenda huenda akabadilika kidogo na hivyo “vivazi vyake

Tusiigeuze simu kuwa bomu la kuvunja ndoa


KAMA kawaida tumekutana kwenye kona yetu ili kujuzana mawili matatu kuhusiana na mahaba.
Nina imani mada yangu ya wiki iliyopita imezua maswali mengi kwa wapenzi juu ya upendo wa kweli ndani ya simu, wengine walifikia hatua ya kuyasema mengine juu ya matatizo ya simu katika uhusiano wao ambao ameingia shetani mvunja amani ndani ya nyumba.
Dada mmoja baada ya kusoma mada ya wiki iliyopita alisema simu ya mumewe imekuwa kama ngozi kwa laazizi wake huyo, kwani kila anapokwenda, hata iwe msalani. Anapobahatika kuipata anakuta ina ‘password’, kitu ambacho anaamini mume wake si muaminifu.
Aliniuliza kuwa mume wake kufanya vile inaashiria nini? Jibu lilikuwa jepesi, si mwanaume hata mwanamke ukiona simu yake ina password au anaichunga sana hata akiwa nyumbani, ujue pale hakuna uaminifu.
Kama nilivyoizungumzia simu wiki jana kuwa makusudia ya mtu aliyeitengeneza kusudio lake kubwa lilikuwa kurahisisha mawasiliano si kingine. Lakini wanadamu wenye mioyo dhaifu tumeitumia kama kichaka cha kuficha maovu yetu.
Sasa hivi ndani ya nyumba simu imekuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani, asiye muaminifu uilinda simu yake kama ikulu ya Barack Obama.
Sasa hivi ndani ya nyumba zetu inaonyesha jinsi gani zimepoteza unaminifu kila mmoja analinda simu yake kuliko hata wivu kwa mwenzake.
Imekuwa kila mmoja anamwinda mwenzake alale ili aipekue simu, kwa vile ni mzoefu hata ukibahatika kuipata utakuta uchafu wake amefuta ili kupoteza ushahidi.
Ukiona hivyo mnakuwa mnaishi kwa mazoea lakini fahamu hakuna upendo ndani ya nyumba yenu na kuvunja ile ahadi ya kuishi kwa upendo na uaminifu katika ndoa.
Unaweka password unamuonyesha nini mwenzako? kama mwanaume unamuonyesha kabisa mkeo kwamba una wengine zaidi yake hapo unamfundisha nini mkeo, akilipa kisasi umlaumu nani?
Hebu turudie somo letu ambalo nimekuwa nikilitoa kila siku ili ambao hawakubahatika kusoma nilipolitoa ili tuangalie unachokifanya ni sahihi na ndiyo mapenzi?
Nilielezea mapenzi ni kupendana kuheshimiana kuoneana huruma kujaliana na uvumilivu.
Nilielezea mapenzi ni kupendana, kuheshimiana, kuoneana huruma, kujaliana na kuvumiliana. Ukiwa na mapenzi lazima utakuwa na vitu hivi kwa mwenzako, pia utakuwa muwazi kwake na mkweli ili kufanya muweze kuishi bila mmoja kuwa na mashaka na mwenzake.
Wapendanao siku zote hulinda heshima yao kwa kila mmoja kuilinda ya mwenzake, pia kuwa wawazi ili chochote kitakachokwenda kinyume, kiulizwe na kupatiwa majibu sahihi bila kujiumauma. Pia huwa hawana mipaka kuanzia katika miili yao na vitu vyote kwa vile huamini wao ni kitu kimoja, hivyo hawafichani kitu.
Watu kama hawa simu si chanzo cha matatizo, bali ni chombo cha mawasiliano, hakuna mtu wa kuificha simu yake wala kuweka password na kila mmoja ana uhuru wa kuishika au kuopokea ya mwenzake.
Nina imani somo langu limesomeka vizuri, sasa tunarudi kwenye mada ya leo kwa kuuliza swali, sifa nilizozieleza kuhusu mapenzi, je, wewe unazo au mwenzako anazo? Je, simu katika nyumba yenu inatumikaje? Ni chanzo cha migogoro au ni chombo cha mawasiliano ambacho kinaachwa popote bila masharti yoyote?
Tutumie simu kama chombo cha mawasiliano, hata kama si muaminifu katika uhusiano, si lazima mwenzako ajue jinsi gani unavyomdharau kupitia simu.
Simu isiwe chanzo cha migogoro na kuvunja nyumba zetu ambazo sasa hivi zimeingia mdudu ambaye ameonyesha jinsi gani tusivyo waaminifu, kitu ambacho kimeongeza ukosefu wa amani katika ndoa zetu.
Tuwe wawazi na wakweli kwa wenzetu, tuone aibu kuonyesha kwa vitendo sisi si waaminifu. Kama ulijua wazuri kuliko mwenzako wapo wengi, ulikaa naye kwa sababu gani?
Kwa leo inatosha, tukutane wiki ijayo.

Wednesday, May 23, 2012

Makosa ambayo hupaswi kuyafanya kwenye uhusiano wa kimapenzi.


KUSHINDWA KUSOMA ALAMA
Zipo alama muhimu ambazo ni vema kuzijua na uzibaini kwa mwenzi wako kabla hujazama kwenye dimbwi la mapenzi. Bahati mbaya wengi hutawaliwa na papara, matokeo yake hushindwa kubaini vitu ambavyo vinaweza kumfanya apate uelekeo wa uhusiano wake.
Katika pointi hii, nashauri watu kwenda kwa mwendo wa kinyonga badala ya kupiga mbizi bila kujua kina cha maji. Kusoma alama muhimu kwa mwenzi wako mapema ni sawa na kutegua kitendawili. Itakusaidia kujua kama kweli uliyenaye ana mapenzi ya kweli au anaweza kuwa laghai.
Wengi wanapoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi hueleza kuwa wanapenda, tena huweka wazi kuwa hisia zimeanguka kwa wale wanaowapenda. Hata hivyo, huacha mambo mengi ndani ya uvungu wa nyoyo zao. Wewe utakuwa mshindi, endapo utaweza kumsoma mwenzi wako na kumuelewa kinagaubaga.
Pointi hapa ni kuwa mwanzo kabisa wa uhusiano, yapo mambo mengi ambayo kila mmoja hujitahidi kuyazungumza. Hiyo huita kujiweka wazi lakini imethibitika kitaalam kwamba maelezo ambayo hutolewa ni asilimia 40 tu, zilizobaki hufichwa. Asilimia 60 zilizobaki utazifichua kwa kusoma alama muhimu.
Nyongeza ni kwamba mara nyingi wengi hujitahidi kusema uongo mwanzoni mwa uhusiano. Hata kama mtu anapenda lakini hudanganya hili na lile pengine kwa hofu, tahadhari au kama pointi ya kushinda penzi. Mantiki hapa ni kukutaka uwe makini na umsome mwenzako kwa undani kabisa.
 Katika kipengele cha kusoma alama muhimu, kuna vitu vya msingi vya kuzingatia ambavyo ni hivi vifuatavyo;

1)    Jamii: Mwenzi wako anasimama vipi na jamii yake? Usiingie kichwakichwa kwenye mapenzi na mtu ambaye hata jamii yake inamuona ni tatizo. Vilevile, yule ambaye ni muoga inabidi uanze kumtia wasiwasi mapema. Ni kwa ajili ya maisha yako, hivyo ni vema kuchangamka.
Hutakiwi kugundua muda umeshapita kuwa mwenzi ana tabia usizopenda. Mapema msome na umuelewe. Chunguza msimamo wake kwenye jamii, anavyojiamini, je, anaonesha kuwa na dira ya maisha. Kama hana uelekeo, unatakiwa kuachana naye haraka.

2)    Hisia: Zisome hisia zake, je ni mtu anayejali? Unatakiwa kujua kama hisia zake zipo karibu kwa kiasi gani. Atakapotakiwa kukutimizia haki yako ya faragha, atakuwa tayari kwa wakati? Ni aibu mmeshakuwa na uhusiano kwa muda mrefu ndiyo unaanza kulalamika kwamba mwenzi wako hakutimizii huduma ya uwanja wa wawili.
Lingine kwenye hisia, unatakiwa ujifunze kujua kama mwenzi wako ni mtu wa kulipuka au kinyume chake. Inawezekana ni kweli mwenzi wako anakupenda lakini akawa ni mtu wa jazba, tatizo dogo ‘anapaniki’ utadhani nyoka aina swila, kakanyagwa mkia. Mjue halafu umpime, je, unaweza kumvumilia? Jiridhishe mara mbili, vinginevyo bwaga manyanga.

3)    Muonekano: Ni kipengele kidogo muhimu ndani ya kifungu cha kushindwa kusoma alama kama sehemu mojawapo inayowafanya wengi kufanya makosa kwenye uhusiano. Muonekano si suala la baadaye, inatakiwa mapema sana umtathmini halafu ujiridhishe kama anakufaa au kinyume chake.
Ni aibu umeshaingia kwenye uhusiano, halafu baadaye unamsaliti mwenzi wako na kuanza kuwatolea macho wale ambao unaona ni wazuri zaidi. Hakikisha kwamba mwanzo kabisa kwenye uhusiano wako, unajiridhisha kuwa anao mvuto unaokutosha.

Itaendelea wiki ijayo.

Yanayoweza kumfanya mumeo atembee na mashosti wako


NI wiki nyingine tena tunakutana kupitia safu hii nakiamini muwazima na mnaendelea vyema na majukumu yenu ya kila siku kama kawaida. Mimi nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwani amekuwa akiniongoza katika kila ninalolifanya katika maisha yangu.
Ndugu zangu, maisha ya kimapenzi yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu sana kwani kuna changamoto nyingi zinazoweza kujitokeza kiasi kwamba usipoangalia unaweza kuishia kusema hutakuja kumpenda mtu, heri uishi peke yako!
Tatizo kubwa ambalo limekuwa likiwasumbua wengi walio kwenye ndoa na wale walio kwenye uhusiano wa kawaida ni usaliti. Uaminifu umepungua kwa kiasi kikubwa, mke wa mtu kutembea na rafiki wa mumewe si kitu cha ajabu siku hizi, mume wa mtu kutembea na mpangaji mwenzake siyo ishu. Nashindwa kuelewa tunaelekea wapi.
Yaani imefika hatua ya mume wa mtu kutembea na ‘hausigeli’ wake tena anafanya hivyo kwenye kitanda anacholala na mkewe, hii si laana jamani? Usiulize kwa nini nimetoa mfano huu, hili limetokea juzi tu kwa mtu wangu wa karibu sana. Alitoka safari na aliporejea usiku akamfumania mumewe akiburudika na ‘hausigeli’, eti mwisho wa siku mwanaume anaomba asamehewe akidai ni shetani kampitia.
Anyway nimeona nianze na hilo ambalo lina uhusiano wa kile ninachotaka kukizungumzia leo. Kama nilivyotangulia kusema hapo mwanzo, imekuwa si jambo la ajabu kusikia mume wa mtu katembea na rafiki wa mke wake.
Wewe utakuwa ni shahidi wa hiki ninachokizungumza kwani kama hakijakutokea basi rafiki yako au ndugu yako kimempata.
Lakini katika uchunguzi wangu nimebaini baadhi ya wake za watu wamekuwa wakitengeneza mazingira ya waume zao kutembea na marafiki zao.
Unaweza kushituka kusikia hivyo lakini ndiyo ukweli wenyewe na utakubaliana na mimi baada ya kusoma vipengele vifuatavyo.
Ukaribu wa mume na marafiki wa mke
Kuna baadhi ya wanawake wamekuwa na tabia ya kuwaweka waume zao karibu sana na marafiki zao. Unakuta mwanamke eti anamruhusu mumewe kwenda klabu au baa na shosti wake. Katika mazingira hayo unatarajia nini?
Sisemi uanze kumfikiria tofauti rafiki yako lakini unachotakiwa kujua ni kwamba, sasa hivi kuna wasichana micharuko ambao ukiwapa nafasi kidogo tu kwa mumeo wanakupindua.
Kwa maana hiyo kitendo cha kumuweka mumeo karibu na mashosti wako unatengeneza mazingira ya kusalitiwa kwa kujitakia hivyo unatakiwa kuwa makini na watu ambao wanastahili kuwa karibu na laazizi wako.
Mawasiliano ya mume na marafiki wa mke
Sisemi marafiki zako wasiwasiliane kabisa na mumeo lakini unatakiwa kuangalia wanawasiliana kwa mambo gani? Utakuwa ni mtu wa ajabu kama utakubali mumeo apigiwe simu au achati na marafiki zako halafu hakuna cha maana wanachoongea, walahi utaula wa chuya!
Unatakiwa kuwa mkali pale unapoona mumeo anawasiliana sana na marafiki zako wa kike kwani waliosalitiwa walianza kuchukulia poa mazingira kama hayo mwishowe wakalia.
Mke kuanika siri za mumewe
Lingine ni tabia ya baadhi ya wanawake kuwasimulia mashosti wao siri ambazo hawastahili kuzitoa nje. Kuna wanawake sijui nisema ni ulimbukeni au ushamba!
Eti unamkuta mke anasimulia mashosti wake jinsi mumewe anavyompa furaha wanapokuwa faragha. Unajiuliza ni kwa nini mtu anafikia hatua hiyo.
Kimsingi hili ni kosa kubwa linalofanywa na baadhi ya wanawake na kujikuta wakikaribisha usumbufu kwa waume zao kutoka kwa wanawake micharuko.
Mwanamke kutochukua nafasi yake
Kwa kifupi mwanamke kushindwa kumdatisha mumewe ni kumfanya aangalie wapi kwingine anakoweza kupatiwa kile anachokihitaji.
Hili liwe fundisho kwa wanawake waliobahatika kuingia kwenye maisha ya ndoa. Kumridhisha mumeo ni kumfanya aepukane na vishawishi vinavyoweza kumfanya akusaliti.
Mpe mapenzi atosheke asifikiria kukusaliti, mpe kila anachokitaka kutoka kwako (ila usimruhusu kuruka ukuta). Hii itamfanya asiwe na tamaa ya kupoteza muda wake kwa marafiki zako ambao ni micharuko wanaotamani kuonja asali yako.

Vumilia, endelea kuwa ‘singo’ kuliko mpenzi pasua kichwa

Na Luqmani Maloto
KILA mtu angeyaheshimu mapenzi, angejua jinsi ya kulinda hisia za mwenzi wake. Angeelewa maana ya kupenda, asigekuwa na shaka pale anapopendwa. Angeishi ndani ya mwenzake, hivyo kuumizana kusingekuwepo, migogoro mikubwa na kuachana isingetokea.
Migogoro mingi inatokea kwa sababu wengi wameyageuza mapenzi kama mchezo (game), hawajui kuwa saikolojia inaonya vitendo vya kuucheza shere moyo wa mtu. Kumfanyia hivyo mtu mwenye hisia za ndani na za kweli katika kupenda unaweza kuua bila kukusudia.
Katika sehemu ya kwanza ya makala haya wiki iliyopita, nilieleza kuwa kama hujawa tayari kupenda, kunyenyekea na kuheshimu ni vizuri ukakaa pembeni kwa sababu unaruhusiwa kucheza game na mtu lakini ni kosa kubwa kucheza game na moyo wa mtu.
Hata hivyo, nilitaka kila mtu awe makini anapokuwa anaingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu. Anapaswa kujihakikishia upendo kutoka moyoni badala ya kujaribu. Wengi walioingia kwa mtindo wa kupima kina cha maji, walilia kwa kusaga meno.
Lipo tabaka ambalo linakuwa limejitosheleza kuwa mapenzi hamna lakini wanang’ang’ania, matokeo yake wanauguza jeraha la moyo kwa muda mrefu. Wengine wakajipa ugonjwa wa moyo. Ni vizuri kuwa makini mno ikiwa unahitaji kupata thamani halisi ya penzi.
Pigania kuhifadhi moyo wako. Uweke katika himaya salama. Usijidanganye kwa penzi lisilo na uelekeo. Lenye sura ya upande mmoja. Wewe unapenda, yeye anakuchora, presha inakupanda na kushuka mwenzako hana habari hata kidogo, tena ikiwezekana atakucheka kama katuni.
 Kuna watu hawaoni umuhimu wa hili, mpenzi maana yake ni msiri wa maisha yako. Unapokuwa umelala fofofo hujitambui, ubavuni kwako yupo yeye. Anaweza kukufanya lolote wakati wewe unaogelea ndotoni. Mpende akupendaye, vinginevyo utakumbana na maumivu yafuatayo;

HATOKUSIKILIZA IPASAVYO
Mapenzi ni hisia. Ni rahisi kwako kujua kwamba uliyenaye anakupenda kwa dhati mnapokuwa mnazungumza. Je, anakusikiliza kiasi gani?
Mtu ambaye hana mapenzi na wewe, hata umwambie kwa lugha gani hawezi kukuelewa. Tena inawezekana ulizungumza naye jana kwa herufi kubwa, lakini leo jua limechomoza anarudia yale yale.
Inawezekana ulimuonya kuhusu tabia ambazo zinakufanya heshima yake ipotee. Hakatazwi kuwa na marafiki wa jinsi nyingine, lakini mazoea yake siyo mazuri kiasi kwamba wanaweza kutembea barabarani wameshikana viuno. Ikiwa unamueleza habadiliki, huyo hakupendi.
Hakusikilizi kwa sababu hana hisia na wewe.

ATAPENDA KUKUFANANISHA
Haamini kama wewe ni mwanamke au mwanaume mwenye mvuto kamili. Akiona wengine barabarani ni rahisi kushawishika. Atajiuliza hivi huyu na wangu vipi? Huyu anaonekana ni mzuri zaidi. Anajiuliza maswali hayo kwa sababu hajakukubali. Shtuka mapema.
Mwanasaikolojia Brandon King katika makala yake: “Be aware with ones heart!” anasema kuwa ni rahisi mtu kujidanganya kwamba aliyenaye siyo chaguo sahihi kwa sababu yupo naye lakini hiyo hutokea kwa mtu ambaye mapenzi yake si asimilia 100.
Anasema: “Vitu vya thamani yeye huvichukulia ni rahisi. Hajui kama mpenzio wake ni wa gharama kubwa. Mtu wa barabarani labda kwa sababu tu amevaa kapendeza, yeye ataanza kumfananisha na mwenzi wake nyumbani na ikiwezekana kumuona bora.
“Wengine hawana uvumilivu, kwahiyo wanaweza kujikuta wakimwaga sifa kwa watu wa pembeni. Wakiendelea huharibu kabisa kwa sababu hujikuta wakiwaeleza hata wapenzi wao, kitu ambacho taaluma ya saikolojia katika eneo la mapenzi inakataza.”
Brandon anaonya: “Ni kosa kubwa kumsifia mtu wa jinsi inayofanana na mwenzi wako mbele yake. Mfano unamwambia mwenzi wako wa kiume kwamba ‘yule kaka mzuri jamani’! Hata kama huna hisia za ndani ya moyo wako lakini haiwezi kumpa picha nzuri, atajiona hayupo salama kwamba unavutiwa na mwingine.
“Fikiria na wewe upande wako. Mwenzi wako anamuona mwanamke na yeye anamwagia sifa, ‘dah yule manzi mrembo, wewe ungekuwa mrembo kama yeye ningejidai sana’! Bila shaka utaumia sana, kwahiyo na yeye ndivyo anavyoweza kupata maumivu.”
Anashauri: “Kila mmoja aridhike kwa jinsi mwenzi wake alivyo. Haikusaidii kitu kumuona bora wa jirani kwani kuna wenzako wanajiuliza huyo wako watampataje? Mheshimu na mtukuze mbele za watu. Ukijenga imani kwamba mpenzi wako ni bora kuliko wote duniani, itakuwa na moyo wako utakubali.

Sunday, May 13, 2012

MAMBO MACHACHE YA KUYAFAHAMU ILI KUEPUKA KUSALITIWA

1.Amini hawezi kukusaliti
Jambo la kwanza kabisa ni kujenga imani kwamba mpenzi wako anakupenda, anakuheshimu na kukuthamini hivyo hawezi kushawishika kwa namna yoyote ile kukusaliti.

Hii itakufanya kuwa na furaha na yeye, pia utamfanyia mambo ya kumfurahisha. Ukiwa huna imani na mpenzi wako, unaweza kujikuta unapunguza mapenzi kwake na matokeo yake ukachochea yeye kuanza kukusaliti.

2.Mtosheleze
Mpenzi wako mchukulie kama mtoto. Unapomlisha unahakikisha ameshiba ndiyo unamuacha. Akitaka pipi unamnunulia. Vivyo hivyo kwa mpenzi wako. Mtoshelezea katika kila nyanja.

3.Muoneshe upendo wa hali ya juu, mpe heshima anayostahili na pale mnapokuwa kwenye mambo yetu yalee, mpe hadi aseme nimeshiba mpenzi wangu. Ukifanya hivyo aende nje kutafuta nini? Akienda, huyo ana tamaa zake za kijinga na ukibaini muache haraka.

4.Zungumza naye
Ndiyo, vunja ukimya, zungumza naye! Si vibaya ukawa unazungumza na mpenzi wako juu ya mambo yahusuyo uhusiano wenu. Muulize ni mambo gani ukimfanyia anasikia furaha, akikuambia na mambo hayo yakawa ndani ya uwezo wako, jitahidi kumtimizia.

5.Muulize, anachukizwa na mambo gani, akikuambia basi jiepushe nayo. Hata asipokuambia, ukimchunguza utayabaini tu.
Hayo ni baadhi tu ya mambo ambayo ukiyazingatia yanaweza kukusaidia katika kumfunga ‘spidi gavana’ kimtindo mpenzi wako ili asikusaliti. Kama itatokea akakusaliti licha ya kumfanyia yote hayo, huyo siyo mtu wa kuendelea kuwa naye.

Moyo ungekuwa wa kioo, wengi tusingekuwa pamoja


NINA imani wote mu wazima kwa uwezo wa Mungu, hali yangu nazidi kumshukuru Muumba kwa kuendelea kunipa upendeleo wa kuendelea kuvuta hewa yake ya bure. Nazidi kukushukuru msomaji kutokana na kuniunga mkono katika kila mada ninayoandika.
Mada ya wiki jana imeonyesha jinsi gani simu zilivyogeuka sumu ya ndoa zetu, kuna mtu alituma ujumbe na kusema, tunakumbuka shuka wakati kumekucha, eti tayari ndoa nyingi zimeshavunjika kwa ajili ya simu.

Namini hatujachelewa, kwani hakuna kipya chini ya jua zaidi ya kukumbushana ili tusiyafanye makosa waliyoyafanya wenzetu, pengine hawakupata nafasi ya kusoma mada hizi kama wewe.
Basi nawe usivunje ndoa yako kwa jambo linaloweza kuepukika na mwisho wa siku useme ungejua. Nina imani nimesomeka vizuri, sasa tuendelee na mada yetu mpya kama inavyosomeka hapo juu.
Nataka nikupe changamoto moja, jiulize hivi “Wanaokaa pamoja wote wanapendana? Jibu lipo wazi, si wote wanaokaa pamoja wanapendana.

Swali lingine: “Kwa nini wapo pamoja mpaka leo hii na wengine wanapata wajukuu na hata kufa pamoja? Najua kabisa kwa akili ya juujuu unaweza ukakataa kwamba kuna watu hawapendani halafu wanaishi pamoja.
Twende pamoja ili kila mmoja aamini kile nitakachokizungumza na fanya uchunguzi kisha utanipa jibu.

Thursday, May 10, 2012

Namna ya kuvaa jioni kulingana na umbo lako

   
KWA kawaida kila mwanamke hutamani kuwa na mvuto wa kutosha hasa anapotoka nyakati za jioni.

Hata hivyo kuna baadhi ya wanawake wanashindwa kufahamu wavae nguo za aina gani ili wawe na mvuto huo kulingana na shepu zao.

Makala haya yanaeleza aina ya nguo ya mhusika kulingana shepu yake.

Mfupi na mwembamba
Usifanye makosa kwa kuvaa gauni ambalo ni kubwa. Jaribu kuepuka magauni marefu au sketi ndefu. Badala yake vaa nguo fupi ambazo zitaonyesha miguu yako, hapo angalau utaonekana �umejazia�.

Vaa viatu virefu iwezekanavyo ili uonekane mrefu.

Kujazia juu na chini (Pear-Shaped)
Kama mwili wako umejaaliwa kujazia juu na chini yaani hipsi kubwa na kifua kipana, utapendeza katika nguo ambayo itakufanya uonekane na kifua chembamba na pia itakayokushika hipsi zao.

Jaribu kuvaa mkanda ulionakshiwa na madini ya fedha au rangi ya dhahabu ili kiuno kionekane.

Kujaa kote (Apple Shape)
Hii ni shepu ambayo mtu anakuwa na makalio manene, tumbo nene, mgongo mpana na kifua kipana. Mtu wa namna hii anatakiwa kuvaa gauni lenye mikono kidogo na lililoungwa chini kidogo ya matiti.

Gauni hilo litaficha tumbo mikono na matiti. Nguo yenye shingo ya �V� inaweza kukufanya uonekane mwembamba kiasi. Lakini pia usiogope kuonyesha miguu yako kwa kuvaa gauni fupi

Umeshindwa kuwa mwaminifu kwa mpenzi wako?

NAKUPONGEZA wewe msomaji mpya wa safu hii. Kama ndiyo unaanza kusoma hapa leo, umechagua sehemu sahihi ya kukuza fikra zako kwenye suala zima la uhusiano, maisha na saikolojia kwa ujumla wake.
Wadau wa kona hii na wale wanaofuatilia kwenye gazeti damu moja na hili, Risasi Mchanganyiko kila Jumatano kwenye safu ya All About Love wanakubaliana na mimi kuwa siku hadi siku maisha yao ya kimapenzi yanakwenda vizuri.
Leo tunajadili eneo muhimu sana katika uhusiano; Uaminifu. Wengi wanaweza kunishangaa kidogo, wakiamini kwamba suala la kuwa mwaminifu linamuhusu mhusika moja kwa moja.
Kwamba kama mtu akitaka kuwa mwaminifu au kinyume chake ni uamuzi wake mwenyewe! Hoja hiyo ni ya kweli, lakini si kwa asilimia zote. Kuna vitu vingine ambavyo vinasaidia kumfanya mtu awe mwaminifu.
Ndugu zangu, wakati mwingine suala la uaminifu si la hiyari! Kuna vitu inabidi vifanyike ili angalau uwe katika wingu la uaminifu, halafu unaongeza na nia yako ya kutaka kuwa mwaminifu, ndipo unafanikiwa.
SAUTI ZA WADAU
Nilipata kuwasiliana na watu wanne wa jinsi tofauti wenye tatizo moja; Wameshindwa kuwa waaminifu. Kutokana na ufinyu wa nafasi, utawasikia wawili kati yao.
Wa kwanza: “Kaka Shaluwa, mimi nina mpenzi wangu ambaye nipo naye kwenye uhusiano, huu mwaka wa tatu. Tunapendana sana. Mimi kama msichana kuna wakati natongozwa na wanaume.
“Kwa sababu ninajua nina mwanaume wangu, huwa nawatosa, lakini wakati mwingine najikuta nakosa nguvu. Nakiri kumsaliti mpenzi wangu mara tatu, ila roho inaniuma sana. Tatizo ni nini kaka yangu? Naomba unisaidie, maana sipendi kumsaliti mpenzi wangu.”
Wa pili: “Mimi ni mwanaume mwenye miaka 37, nimeoa na nina watoto wawili na mke wangu mpenzi. Nimemfuatilia sana, kiukweli ni mwaminifu kupindukia. Hata mimi napenda sana kuwa kama yeye, lakini ndiyo hivyo, nashindwa. Nimeshatoka na wasichana wawili, sipendi kabisa hali hii.”
FUNZO
Kwa maelezo yao, tunaona namna ambavyo watu hao ambao wapo kwenye uhusiano (mwingine kwenye ndoa) lakini wanawasaliti wenzi wao. Hata hivyo, si kwa kupenda – wanafanya hivyo na moyoni wanaumia.
Jiangalie na wewe rafiki yangu mpenzi. Unamheshimu mpenzi/mwanandoa mwenzako kwa kuwa naye peke yake au unamsaliti? Hebu angalia ndani ya nafsi yako, ni jambo unalopenda kulifanya au linakuumiza?
Sikia rafiki yangu, usaliti ni sumu ya mapenzi. Ni mwanzo wa kumkosoa mpenzi wako na kuziona kasoro zake. Habari zaidi ni kwamba, mtu anayechanganya sana wapenzi ni rahisi kupoteza uwezo wa kupenda.
Hujikuta akiwachukia watu wa jinsi ya pili, huongozwa zaidi na tamaa na msisimko wa mapenzi hupungua. Zipo athari nyingine nyingi zinazotajwa kisaikolojia kwa mtu asiye mwaminifu. Wanasaikolojia wanakwenda mbali zaidi – wanasema si ajabu mhusika kuanza kupoteza imani na hata yeye mwenyewe. Hajiamini tena.
UNATAKA KUWA MWAMINIFU?
Huu ndiyo mwongozo wako katika somo hili. Kwa maneno mengine, kama wewe ni msaliti na unapenda tabia yako, ishia hapa. Usiendelee kusoma hii mada maana haikufai. Inawezekana ni mwaminifu na unatamani kuendelea kudumu katika uaminifu wako, ni jambo zuri na mada hii ni kwa ajili yako. Twende tukaone sasa.

WEKA NIA
Si uchawi, ni imani ya ndani ya moyo wako. Kila kitu kinaanza na nia. Kama ni kweli unatamani kuwa mwaminifu kwa mwenzi wako, anza kujenga hili kuanzia moyoni mwako. Jiambie kuwa unapenda kuwa mwaminifu siku zote na unatamani kuendelea hivyo.
ANZA NA KINYWA
Hili ni jambo la kwanza kabisa kwako wewe ambaye unahitaji kuwa mwaminifu. Nimesema tangu mwanzo kuwa unaweza kuwa na nia ya kutaka kuwa mwaminifu, lakini ukaangushwa na mambo madogo ambayo yatakufanya baadaye ujute.
Kinywa chako ni kitu muhimu sana kuzingatia. Pima maneno yako. Usipende kuzungumza lugha chafu, maneno yasiyofaa au stori za mapenzi (hasa na watu wasio wa jinsia yako).
Inawezekana usione umuhimu wa hili, lakini rafiki yangu, nikuambie kitu kimoja? Unapoweka mazoea ya kuzungumza na marafiki zako mambo ya mapenzi, ni rahisi sana kujiingiza kwenye usaliti.
Utaanza kama burudani, mipaka ikishavukwa utajiona sehemu ya stori zenu. Namaanisha unaweza ukatamani au kuvaa uhusika wa stori yenyewe, hapo sasa inakuwa rahisi kuingilika hata kama nia yako haikuwa hiyo.
Zungumza kwa busara, achana na utani usio na maana. Kinywa chako kioneshe namna unavyojiheshimu. Kama una mazoea ya kujenga utani sana, ni rahisi mtu kukujaribu kimapenzi, akiwa na ngao ya utani!
Ukikubali amekubeba, ukikataa anakuambia: “Nilikuwa nakutani bwana...hutaniwi wewe?”
Umeona eeh?!
Basi sawa...ngoja nipumzike hapa kwa leo. Endelea kuyatafakari haya, wakati ukisubiri wiki ijayo kwa mwendelezo wake.